Pata taarifa kuu

Waziri wa mambo ya kigeni wa Ufaransa anazuru Kyiv

Nairobi – Waziri mpya wa mambo ya nje wa Ufaransa Stephane Sejourne yuko jijini Kyiv, hii ikiwa ni ziara yake ya kwanza rasimi  nje ya nchi.

Ziara yake inkuja wakati huu washirika wa Kyiv wakiendelea kutafuta njia za kuendelea kusimama na Ukraine
Ziara yake inkuja wakati huu washirika wa Kyiv wakiendelea kutafuta njia za kuendelea kusimama na Ukraine AFP - LUDOVIC MARIN
Matangazo ya kibiashara

Wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanasema hatua hii ni njia moja ya Ufaransa kuonyesha kuendelea kusimama na Ukraine dhidi ya uvamizi wa Urusi.

Ziara yake inkuja wakati huu washirika wa Kyiv wakiendelea kutafuta njia za kuendelea kusimama na Ukraine, suala la ufadhili likipewa kipau mbele.

Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa kwenye ukurasa wa X, zamani ukijulikana kama Twitter na wizara yake, Stephane Sejourne aliwasili Kiev kwa ziara yake ya tangu kuteuliwa kwa nafasi hiyo kuendeleza juhudi za kidiplomasia za Ufaransa huko na kusisitiza kujitolea kwa Ufaransa kwa washirika wake na kwa raia wa Ukraine.

Sejourne, ambaye alichukua nafasi ya Catherine Colonna katika mabadiliko ya serikali siku ya Alhamisi, anatarajiwa kukutana na Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky.

Sejourne, 38, ambaye tofauti na Colonna hana historia ya kuwa mwanadiplomasia kitaaluma, ni mshirika wa karibu wa Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron na katibu mkuu wa chama cha rais cha Renaissance.

Tayari alikuwa ameahidi kuendelea kuunga mkono Ukraine, ambayo imekuwa imekuwa vitani na nchi ya Urusi kwa karibu miaka miwili, alipochukua rasmi madaraka Ijumaa.

Stephane Sejourne alichukua nafasi yake Catherine Colona
Stephane Sejourne alichukua nafasi yake Catherine Colona © via Reuters

Msaada wa kijeshi wa Ufaransa kwa Ukraine ni sawa na euro bilioni 3.2 (dola bilioni 3.5), kulingana na ripoti ya bunge iliyochapishwa mnamo Novemba.

Rais Zelensky alionya kuwa ucheleweshaji wowote wa misaada unaweza kuathiri vibaya mwenendo wa vita.

Pia amesisitiza kuwepo kwa ulinzi zaidi wa anga, kwani nchi yake imekuwa ikikabiliwa na mashambulio mapya ya angani kutoka Urusi.

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky ameendelea kushinikiza nchi washirika wake kuihami nchi yake
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky ameendelea kushinikiza nchi washirika wake kuihami nchi yake AP - Efrem Lukatsky

Haya yanajiri wakati huu Urusi ikirusha makombora 40 na ndege zisizo na rubani nchini Ukraine usiku kucha.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.