Pata taarifa kuu

Ufaransa: Waandamanaji elfu moja wamekamatwa, ghasia zaidi zikiripotiwa

Nairobi – Matukio ya ghasia na uporaji yameshuhudiwa kwa usiku wa nne wa maandamano nchini Ufaransa wakati huu maofisa wa polisi wakithibitisha kukamatwa kwa watu elfu moja wanaoandamana kufuatia kifo cha kijana aliyeuawa na afisa wa usalama katika kituo cha trafiki.

Polisi wanasema wamewakamata waandamanaji elfu moja
Polisi wanasema wamewakamata waandamanaji elfu moja © AP / Lewis Joly
Matangazo ya kibiashara

Kwa mujibu wa serikali,  ghasia hizo "zimepungua" ikilinganishwa na usiku uliopita, lakini wizara ya mambo ya ndani bado iliripoti kukamatwa kwa watu 994 kote nchini kwa usiku mmoja, na majeruhi 79,  polisi na askari wakiwa miongoni mwao.

Maandamano nchini humo yaliaanza siku ya  Jumanne, baada ya kuchochewa na kifo cha Nahel mwenye umri wa miaka 17 ambaye alipigwa risasi na afisa wa polisi.

Mamake Nahel, kijana aliyeuawa ni miongoni mwa waandamanaji waliojitokeza kukashifu kitendo hicho
Mamake Nahel, kijana aliyeuawa ni miongoni mwa waandamanaji waliojitokeza kukashifu kitendo hicho REUTERS - SARAH MEYSSONNIER

Mamlaka nchini humo katika taarifa yake imeeleza kuwa licha ya kuripotiwa kwa majeruhi katika maandamano hayo, magari 1,350 na majengo 234 yamechomwa moto.

Makabiliano yameripotiwa licha ya Ufaransa kuwatuma maafisa 45,000, hii ikiwa ni idadi  kubwa zaidi kutumwa kuwakabili waandamanaji.

Maofisa wa polisi wametumwa kuwazuia maandamano yenye ghasia
Maofisa wa polisi wametumwa kuwazuia maandamano yenye ghasia © REUTERS / PASCAL ROSSIGNOL

Waandamanaji wameripotiwa kupora mali katika  miji ya Marseille, Lyon na Grenoble ambapo pia ghasia zaidi zimeripotiwa.

Timu ya taifa ya soka ya Ufaransa nayo pia imetoa wito kwa kusitishwa kwa vurugu zinazoendelea kushuhudiwa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.