Pata taarifa kuu

Ufaransa: Macron aahidi mswada kuhusu uavyaji mimba katika Katiba

Katika hafla ya Siku ya Kimataifa ya Haki za Wanawake, Jumatano hii, Machi 8, Emmanuel Macron ametoa pongezi za kitaifa kwa wakili wa masuala ya wanawake Gisèle Halimi. Katika jengo la mahakama ya Paris, rais wa Ufaransa pia ametangaza kwamba atawasilisha mswada, "katika miezi ijayo", kujumuisha utoaji wa mimba kwa hiari katika Katiba. Neno linalosubiriwa kwa hamu na vyama vya wanawake.

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron akitoa hotuba ya kumuenzi mwanasiasa wa kike na mwanasheria wa Ufaransa Gisèle Halimi, Jumatano hii Machi 8, 2023 mjini Paris.
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron akitoa hotuba ya kumuenzi mwanasiasa wa kike na mwanasheria wa Ufaransa Gisèle Halimi, Jumatano hii Machi 8, 2023 mjini Paris. AP - Michel Euler
Matangazo ya kibiashara

Baraza la Bunge na kisha Bunge la Seneti ziliidhinisha kujumuishwa kwa utoaji wa mimba kwa hiari (IVG) katika Katiba.

Baada ya kutoa heshima zake kwa Gisèle Halimi, rais wa Ufaransa kwa hiyo anaanzisha hatua inayofuata: “Gisèle Halimi, amesema rais Macron, kwa maneno yake, alibadilisha sheria. Na leo nataka nguvu ya ujumbe huu itusaidie kubadili Katiba yetu, ili kuweka nakshi ya uhuru wa wanawake kuamua kutoa mimba kwa hiari. "

Kwa kuhakikisha kwa dhati kwamba hakuna kitu kinachoweza kuzuia au kutengua kile ambacho hakiwezi kutenduliwa; pia kutuma ujumbe wa kimataifa wa mshikamano kwa wanawake wote ambao leo wanaona uhuru huu umekiukwa...

'Uhuru' wa kutoa mimba, badala ya 'haki'

Uhuru, neno lililochaguliwa na Emmanuel Macron ni muhimu. Ni lile ambalo maseneta wa mrengo wa kulia walipendelea, huku wabunge wakitetea dhana ya haki ya kuavya mimba.

Lakini kwa mkuu wa wabunge wanaounga mkono sera ya Macron, Aurore Bergé, jambo kuu ni ahadi ya rais. "Kilicho muhimu, kulingana na mbunge huyo, ni kuwa ahadi hii kutoka kwa Rais wa Jamhuri  iko wazi na ambayo inamaanisha kwamba kwa mara nyingine tena, tumeonyesha kuwa kuna njia na katika Baraza la Bunge na katika Bunge la Seneti, kwa hivyo ndio, ninaamini kwamba ni wakati wa kihistoria ambao tulipitia na kwamba tutapitia, naamini, hivi karibuni sana na kupitishwa katika Bunge marekebisho haya ya Katiba. »

Mshauri wa Emmanuel Macron anafafanua: kuzungumza juu ya uhuru wa kutoa mimba ni jambo linalokubaliwa zaidi. Kwa sababu rais wa jamhuri atahitaji nusu asilimia 60kura ya Bunge ili kurekebisha Katiba, ikiwa ni pamoja na sauti moja ya upinzani.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.