Pata taarifa kuu
URUSI- UKRAINE- MAPIGANO

Mawaziri wa ulinzi kutoka Jumuiya ya NATO wakutana Brussels

NAIROBI – Mawaziri wa ulinzi kutoka jumuiya ya NATO pamoja na Marekani, wamekubaliana kuongeza kasi ya kuisaidia silaha zaidi nchi ya Ukraine, wakati huu Urusi ikizidisha mashambulio mashariki mwa nchi hiyo.

Mawaziri wa ulinzi wa nchi za Jumuiya ya NATO wamekutana jijini Brussels wakiahidi kutoa usaidizi zaidi kwa Ukraine
Mawaziri wa ulinzi wa nchi za Jumuiya ya NATO wamekutana jijini Brussels wakiahidi kutoa usaidizi zaidi kwa Ukraine REUTERS - JOHANNA GERON
Matangazo ya kibiashara

Katika kikao chao cha Brussels, Ubelgiji, mawaziri hao wamesema Urusi itaendelea kufanya kosa kama inafikiria nchi hizo zitasitisha msaada wake kwa Ukraine, na kwamba hivi karibuni nchi zao zitatuma silaha zaidi.

Lloyd Austin, ni waziri wa ulinzi wa Marekani.

“Tulichukua hatau kwa haraka, haraka ambayo ilihitajika kwa wakati husika na mara zote imetutaka tuchukue hatua kwa vile tulivyoahidi kwa Ukraine. ”amesemaLloyd Austin, ni waziri wa ulinzi wa Marekani

Mkutano huu unakuja wakati huu Ukraine ikitoa wito kwa washirika wake kutuma silaha zaidi zikiwemo za masafa marefu na ndege za kivita ilikupiga jeki azma yake ya kujilinda kutokana uvamizi wa Urusi nchini wake.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.