Pata taarifa kuu
UFARANSA- UCHUMI

Ufaransa, vyama vya wafanyikazi kushiriki migomo zaidi wiki ijayo

Nchini Ufaransa, vyama vya wafanayazi, vimetangaza migomo mingine miwili wiki ijayo kuendelea kupinga sera ya Pensheni ya Serikali ya rais Emmanuel Macron. 

Wafanyikazi wa umma wameshiriki maandamano nchini Ufaransa kupinga mpigano ya rais Macron ya kuongeza umri wa kustaafu.
Wafanyikazi wa umma wameshiriki maandamano nchini Ufaransa kupinga mpigano ya rais Macron ya kuongeza umri wa kustaafu. REUTERS - BENOIT TESSIER
Matangazo ya kibiashara

Jumanne, shughuli za masomo, usafiri na huduma nyingine za umma nchini zilitatizika kufuatia hatua ya maelfu ya wafannyakazi kujitokeza katika miji mbalimbali kupinga mpango wa rais Macron, kupinga ongezeko la umri wa kustaafu kutoka miaka 62 hadi 64. 

Aliyekuwa mgombea urais, mwaka uliopita Jean-Luc Mélenchon aliungana na waandamanaji kupinga mabadiliko hayo. 

“Bila shaka rais Macron anapoteza kila ambacho anafanya ni kutupotezea muda.”ameeleza Jean-Luc Mélenchon.  

Rais Emmanuel Macron, amesisitiza kuwa hatabadili msimamo wake licha ya maandamano yanayoendelea. 

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.