Pata taarifa kuu
URUSI-UKRAINE

Watu zaidi ya 20 wauawa nchini Ukraine baada ya kushambuliwa na jeshi la Urusi

Watu zaidi ya 20 wameuawa wakiwemo watoto wawili baada ya jeshi la Urusi kurusha kombora katika makaazi ya watu Kusini Magharibi mwa jimbo la Odesa nchini Ukraine.

Shambulizi la bomu katika makaazi ya watu jimboni Odesa
Shambulizi la bomu katika makaazi ya watu jimboni Odesa REUTERS - STRINGER
Matangazo ya kibiashara

Maafisa wa serikali nchini Ukraine wamesema kombora la Urusi lililenga  jumba moja lenya maakazi la  orofa 9 na  mkahawa na na kuwaua  19 hao mbali na kusabisha moto mkubwa, ambpo shughuli za kuwaoakoa waliokwama kwenye vifusi zilianza amara moja.

Jeshi la Ukraine limetuhumu Urusi kwa kutumia makombora kushambulia miji yake katika mashambulizi yake ya hivi karibuni, likiwemo shambulizi la  Kremenchuk ambapo watu 18 walifariki na lile la jiji la Kyiv jumapili iliopita.

Andriy Yermak mkuu wa  wafanyakazi katika afisi ya rais wa Ukraine, amefaninisha tukio la Ijumaa na magaidi amabao wameshindwa katika uwanja wa mapambano na sasa wanawashambulia raia ambao hawana hatia.

Hata hivyo msemaji wa Krimlin, Dmitry Peskov, amekanusha taarifa za jeshi la Urusi kushambulia raia akisema wanajeshi wa Urusi siku zote hawafanyi kazi na raia.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.