Pata taarifa kuu
MZOZO WA UKRAINE-URUSI

Urusi yasema inasitisha vita kwa siku tatu katika eneo la kiwanda cha Azovstal

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky ametoa wito kwa Umoja wa Mataifa kusaidia kuokoa maisha ya raia wa nchi hiyo waliojeruhiwa na wanaosalia katika kiwanda kikubwa cha kutengeza vyuma  katika eneo la Azovstal, mjini Mariupol.

Des civils évacués de l'usine assiégée d'Azovstal sous le regard de soldats russes le 1er mai 2022.
Des civils évacués de l'usine assiégée d'Azovstal sous le regard de soldats russes le 1er mai 2022. REUTERS - ALEXANDER ERMOCHENKO
Matangazo ya kibiashara

Zelensky ametoa wito huo baada ya kuzungumza na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guteress kwa njia ya simu baada ya baadhi ya watu kuokolewa.

Urusi imesema itasitisha mashambulio katika êneo hilo kwa siku tatu zijazo ili kuwaruhusu raia waliokwama kupelekwa katika maeneo salama.

L'armée russe a lancé mardi 3 mai un assaut contre l'usine Azovstal à Marioupol, où sont encore retranchés des civils et des soldats ukrainiens.
L'armée russe a lancé mardi 3 mai un assaut contre l'usine Azovstal à Marioupol, où sont encore retranchés des civils et des soldats ukrainiens. © REUTERS - ALEXANDER ERMOCHENKO

Matukio ya msingi kuhusu mzozo unaoendelea:

-Vita vimesitishwa katika eneo la Azovstal kwa siku tatu, kuwaruhusu watu kukimbilia katika maeneo salama.

-Ukraine inasema watu zaidi ya 300 wameondolewa kutoka mjini Mariupol siku Jumatano, maisha ya wengine waliosalia yapo hatarini.

-Urusi inasema, jeshi lake limefanya mazoezi ya kurusha makombora ya nyuklia, katika Bahari ya Baltic, iliyo kati ya nchi ya Poland na Lithuania.

-Rais wa Marekani Joe Biden amesema yupo tayari kuiwekea Urusi vikwazo zaidi na atajadiliana na viongozi wenzake kutoka nchi tajiri za G7.

-Ukraine, inaishtumu Urusi kwa kupanag kuwa na gwaride la kijeshi katika mji wa Mauripol, Mei 9, siku ambayo Moscow inakumbuka ushindi dhidi ya wapiganaji wa Kinazi baada ya vita vya pili vya dunia.

-Ripoti zinasema, taarifa za Kiinteljensia, zilizotolewa kwa jeshi la Ukraine kutoka kwa Marekani, zilisaidia wanajeshi wa Ukraine kuwashambulia na kuwauwa Majenerali angalau 12 wa Urusi.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.