Pata taarifa kuu
UFARANSA-DIPLOMASIA

Macron aendelea kupata pongezi mbalimbali kutoka kwa viongozi duniani

Viongozi mbalimbali duniani, wamempongeza rais Macron kwa ushindi alioupata. Miongoni mwa pongezi hizo zimetoka barani Ulaya kutoka kwa rais wa Tume ya Umoja wa Ulaya Ursula von der Leyen na rais wa Baraza hilo Charles Michel ambao wamesma wana uhakika wa ushirikiano wa Ufaransa miaka metano ijayo. 

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron akipunga mkono jukwaani baada ya kuchaguliwa tena kuwa rais, baada ya kutangazwa matokeo ya duru ya pili ya uchaguzi wa urais wa mwaka 2022, Paris, Ufaransa, Aprili 24, 2022.
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron akipunga mkono jukwaani baada ya kuchaguliwa tena kuwa rais, baada ya kutangazwa matokeo ya duru ya pili ya uchaguzi wa urais wa mwaka 2022, Paris, Ufaransa, Aprili 24, 2022. REUTERS - GONZALO FUENTES
Matangazo ya kibiashara

Kansela wa Ujerumanu Olaf Scholz naye amesema kwa ushindi wa Macron, wapiga kura nchini Ufaransa wametuma ujumbe, kuwa wanaiamini Umoja wa Ulaya. 

Rais wa Marekani Joe Biden naye amemwambia Macron kuwa, anatumai kuendeleza ushirikiano kati ya mataifa hayo mawili, ujumbe kama huo pia ukitoka kwa Xi Jinping wa China. 

Salamu za pongezi pia zimetoka kwa rais wa Ukraine, Volodymyr Zelensky  ambaye amesema ana imani kuwa wataendeleza ushirikiano ili kupata ushindi. 

Naye rais wa Urusi Vladimir Putin kupitia ukurasa wake wa Telegram, amempongeza Macron na kumtakia afya njema. 

Viongozi wa  mataifa ya Afrika, wakiongozwa na rais wa Senegal ambaye  pia ni Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika Macky Sall , Paul Kagame wa Rwanda, Samia Suluhu Hassan wa Tanzania, Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed ni miongoni mwa viongozi waliompongeza Macron kwa ushindi aliopata. 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.