Emmanuel Macron: Niko tayari kulitumikia taifa kwa maslahi ya raia wote
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron, baada ya kuchaguliwa tena kuongoza nchi hiyo kufuatia ushindi dhidi ya mpinzani wake Marine Le Pen, ameapa kuanza kazi ngumu ya kuliunganisha taifa hilo lililogawanyika kisiasa.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Macron aliyepata ushindi wa asilimia 58.54 dhidi ya Le Pen aliyepata asilimia 41.46, amesema atakuwa rais wa wote.
Licha ya kushindwa, Le Pen amesema chama chake kimeshinda na sasa nguvu zinaelekezwa kwenye uchaguzi wa wabunge mwezi Juni.
Macron anakuwa rais wa kwanza kuchaguliwa kwa mihula miwili nchini Ufaransa, baada ya miaka 20.