ITALIA
Zaidi ya wahamiaji 400 wawasili Lapeduza Italia
Boti nne zilizowabeba zaidi ya wahamiaji 400 zimewasili katika Kisiwa cha Lampedusa, chini Italia baada ya kukamatwa na mamlaka ya Italia katika eneo hilo la pwani ya Bahari ya Mediterania
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Kulingna na shirika la habari la Italia ANSA, moja kati ya boti hizo, iliyowapakia watu 325, ilizuiwa umbali wa mile 8 kutoka Lampedusa.
Boti nyingine ikiwa na watu 90 ilikamatwa na polisi inayodhibiti ukwepaji wa kodi sambamba na yongine mbili, moja ikiwa na abiria 98 na nyingine watu 16.
Kisiwa cha Lampedusa kimekuwa eneo kuu la kuingilia Ulaya kwa wahamiaji wengi na hasa kutoka katika mataifa ya Tunisia na Libya.