Pata taarifa kuu
UFARANSA

Kesi ya kwanza ya aina mpya ya Corona chathibitishwa Ufaransa

Ufaransa imerekodi kesi ya kwanza ya aina mpya ya virusi vya Corona iliyoanzia nchini Uingereza. Mtu huyo aliyeabukizwa kirusi hicho alipatikana huko Tour, Wizara ya Afya imetangaza siku ya Ijumaa usiku.

Baada ya miezi mitatu ya kupungua kwa visa vya maambukizi, tangu kiwango cha juu kama hicho kufikiwa mwishoni mwa mwezi Julai, idadi ya kila siku ya maambukizi imeongezeka tena nchini Brazil.
Baada ya miezi mitatu ya kupungua kwa visa vya maambukizi, tangu kiwango cha juu kama hicho kufikiwa mwishoni mwa mwezi Julai, idadi ya kila siku ya maambukizi imeongezeka tena nchini Brazil. REUTERS
Matangazo ya kibiashara

Mtu aliyeambukizwa ni raia wa Ufaransa anayeishi nchini Uingereza. ameonekana na dalili za aina hiyo mpya ya Ugonjwa aw COVID-19 na amewekwa karantini nyumbani kwake, imesema taarifa.

Mfaransa huyo aliyewasili "kutoka London mnamo Desemba 19", "anapewa matibabu katika hopitali ya CHU tangu Desemba 21 baada ya kupatikana na maambukizi ya virusi hivyo", imesema Wizara ya Afya, ambayo imehakikisha kwamba ni "kisa cha kwanza cha maambukizi ya aina mpya ya virusi vya Corona ” ambacho kimegunduliwa nchini Ufaransa.

"Mamlaka ya afya inaendelea kutafuta wahudumu wa afya ambao walikuwa wakimhudumia mgonjwa huyo na watu waliotangamana naye, ili waweze kuwekwa karantini, ili kudhibiti kuenea kwa aina hiyo pya ya virusi vya Corona, ambavyo ni hatari binadamu", kimesema kituo cha kudhibiti na kuzuia magonjwa nchini Ufaransa.

Kisa kama hicho kimeripotiwa nchini Ujerumani, ambaye ni mwanamke aliyewasili kwa ndege kutoka London, na pia nchini Lebanoni kisa kingine kimethibitishwa kwa abiria aliyetokea London, nchini Uingereza.

Mataifa ya Uhispania, Italia na Uholanzi pia yametangaza visa hivyo.

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.