Arsenal kuwakosa wachezaji wake Fabregas na Nasri
Wachezaji wawili wa timu ya Arsenal ambao ni Cesc Fabregas ambae amekubali kujilipia sehemu ya pesa ilioombwa na club yake na kufuta deni alilokuwa akidai kutoka Arsenal ilimradi tu aondoke na kwenda kuichezea timu ya Barcelone, Huku Samir Nasri akikubaliwa kuelekea manchester City.
Imechapishwa:
Hata hivyo katika mahojiano na vyombo vya habari manaja wa club ya Arsenal Arsene Wenger hakuthitisha kuondoka kwa wachezaji hao wawili lakini amesema hawatokuwemo katika kikosi chake kitachopambana siku ya jumamosi na New Castlle.
Weka hakukanusha habari iliondikwa na magazeti nchini uingereza kuhusu kuondoka kwa wachezaji hao 2 lakini amesema hakusikitishwa na hatuwa ya wachezaji hao 2 kuomba kuondoka katika klabu hiyo
Wakati huohuo Sesc Fabregas anaelekea Uhespania ambapo atatambulishwa mbele ya mashabiki wa Barcelona siku ya jumamosi.