Ufaransa
Mkuu wa IMF Christine Lagarge matatani kwa ufisadi
Mahakama nchini Ufaransa imeamuru ufanywe uchunguzi dhidi ya mkurugenzi Mkuu wa shirika la fedha duniani IMF Christine Lagarge.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Mahakama hiyo imeagiza uchunguzi huo ufanywe dhidi yake kutokana na tuhuma za ufisadi alipokuwa waziri wa fedha nchini humo.
Lagarde anatuhumiwa kuwa alishinikiza benki mmoja nchini humo kutoa fedha ili kufadhili kampeni za rais Nicolas Sarkozy katika uchaguzi wa rais nchini Ufaransa.
Hata hivyo Lagarde amekana kufanya kosa lolote na wachambuzi wa mambo wanahisi kuwa tuhuma hizi zinaweza kumharibia wasifu wake kama Mkurugenzi Mkuu wa IMF.