Norway
Mtuhumiwa wa mauaji ya watu 77 nchini Norway atowa mapendekezo kadhaa wakati kesi yake ikiendelea
Mwanaume mmoja, aliyekiri kuwaua vijana 77 mwishoni mwa mwezi uyliopita jijini Oslo nchini Norway, ametoa mapendekezo kadhaa anayotaka kufanyiwa kazi wakati kesi yake ikiendelea ikiwa ni pamoja na kujizulu kwa serikali ya Norway na mtaalam atakayemchunguza ikiwa ana matatizo ya akili, atoke Japan.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Wakili wa mwanaume huyo Anders Behring Breivik mwenye umri wa miaka 32, Geir Lippestad amesema kutoka na mahitaji ya mteja wake,ni wazi kuwa ana matatizo ya akili.
Tayarai serikali ya Norway ilikuwa imewapa kazi madakatari wawili kufanya uchunguzi wao na kutoa mapendekezo yao kufikia tarehe moja mwezi Novemba .