Pata taarifa kuu

Jeshi la Israeli laendeleza mashambulio kwenye mji wa Rafah, Gaza

Nairobi – Jeshi la Israeli limeendeleza mashambulio ya angaa dhidi ya kundi la Hamas kwenye mji wa Rafah huko Gaza, wakati huu likijiandaa kuanza operesheni ya ardhini kwenye mji huo.

Tangu kuanza kwa vita kati ya Jeshi la Israeli na kundi la Hamas tangu Oktoba 7 mwaka uliopita, watu wanaokadiriwa kuwa 1,160 wameuawa nchini Israeli hiy wengine karibu Elfu 28 wakiuawa kwenye ukanda wa Gaza
Tangu kuanza kwa vita kati ya Jeshi la Israeli na kundi la Hamas tangu Oktoba 7 mwaka uliopita, watu wanaokadiriwa kuwa 1,160 wameuawa nchini Israeli hiy wengine karibu Elfu 28 wakiuawa kwenye ukanda wa Gaza AFP - MAHMUD HAMS
Matangazo ya kibiashara

Viongozi wa Hamas kwenye ukanda wa Gaza wanaonya kuwa mpango  huo wa jeshi la Israeli, utasababisha mauaji na majeraha makubwa kwa raia wa kawada kwenye eneo hilo la Rafah, lenye watu wengi.

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu REUTERS - RONEN ZVULUN

Siku ya Ijumaa, Waziri Mkuu wa Israeli Benjamin Netanyahu, aliwaambia Mawaziri kuwasilisha mpango wa kuwaondoa wananchi kwenye mji huo kabla ya kutumwa kwa vikosi vya ardhini.

Mpango huu umelaaniwa na rais wa mamlaka ya Palestina, Mahmoud Abbas, ambaye amesema hatua ya Israeli inatishia usalama na amani ya kikanda na inavuka mstari mwekundu.

Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani akiwa na rais wa mamlaka ya Palestine
Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani akiwa na rais wa mamlaka ya Palestine REUTERS - EVELYN HOCKSTEIN

Saudi Arabia nayo imeonya kuwa iwapo Israeli itaendelea na mpango wake, itababisha janga kubwa la binadamu katika ukanda wa Gaza na kulitaka Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuingilia kati.

Tangu kuanza kwa vita kati ya Jeshi la Israeli na kundi la Hamas tangu Oktoba 7 mwaka uliopita, watu wanaokadiriwa kuwa 1,160 wameuawa nchini Israeli na wengine karibu elfu 28 wakiuawa kwenye ukanda wa Gaza.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.