Pata taarifa kuu

ICJ kutoa uamuzi kuhusu madai ya Israel kutekeleza mauaji ya kimbari Gaza

Nairobi – Majaji wa Mahakama ya kimataifa ya haki ICJ, leo watatoa uamuzi wao wa awali kuhusu kesi iliyowasilishwa na Afrika Kusini, ikiishtaki Israeli kwa kutekeleza mauaji ya kimbari kwenye ukanda wa Gaza.

Majaji wa Mahakama ya kimataifa ya haki ICJ, leo watatoa uamuzi wao wa awali kuhusu kesi iliyowasilishwa na Afrika Kusini.
Majaji wa Mahakama ya kimataifa ya haki ICJ, leo watatoa uamuzi wao wa awali kuhusu kesi iliyowasilishwa na Afrika Kusini. © Amir Cohen / Reuters
Matangazo ya kibiashara

Mahakama hiyo haitarajiwi kutoa hukumu dhidi ya Israeli na kuamua iwapo jeshi lake linatekeleza mauaji ya kimbari dhidi ya raia wa Palestina kwenye ukanda wa Gaza au la.

Kinachotarajiwa kutokea ni kuwa, huenda Majaji hao wakaimbia Israeli kuachana na operesheni zake za kijeshi kwenye eneo la Gaza, ambazo zimekuwa zikiendelea tangu Oktoba 7 mwaka uliopita, au kuruhusu misaada ya binadamu kuwafikia wanaothiriwa na vita hivyo.

Israel imekuwa ikipambana na wapiganaji wa Hamas katika ukanda wa Gaza
Israel imekuwa ikipambana na wapiganaji wa Hamas katika ukanda wa Gaza REUTERS - IBRAHEEM ABU MUSTAFA

Ripoti zinasema kuwa, katika hatua hii, Majaji watatoa maelekezo kuhusu kesi hiyo, kabla ya baadaye kutoa mtazamo wake kuhusu iwapo, mauaji ya kimbari yanatokea kwenye ukanda wa Gaza, mchakato ambao unaelezwa utachukua miaka.

Katika kesi hiyo, Afrika Kusini inaishtumu Israeli kwa kukiuka kifungu cha  mkataba wa Umoja wa Mataifa wa mwaka 1948, dhidi ya mauaji ya halaiki.

Mamia ya raia wameripotiwa kutoroka katika eneo la Gaza wakihofiwa kushambuliwa na Israel
Mamia ya raia wameripotiwa kutoroka katika eneo la Gaza wakihofiwa kushambuliwa na Israel REUTERS - IBRAHEEM ABU MUSTAFA

Hata hivyo, Israeli imekanusha madai ya Afrika Kusini, kwa kile inachosema kuwa nchi hiyo imekosa hoja na haielewi kinachotokea, na ilichofanya ni kupotosha ukweli wa operesheni yake kwenye ukanda wa Gaza.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.