Pata taarifa kuu
UTURUKI- SYRIA

UN : Watoto milioni 7 Syria, Uturuki wanahitaji msaada

NAIROBI – Shirika la afya duniani, WHO, linasema tetemeko la ardhi lililoikumba nchi ya Uturuki na Syria wiki iliyopita, ni baya zaidi kuwahi kushuhudiwa kwenye ukanda wa Ulaya katika kipindi cha zaidi ya miaka 100.

Umoja wa mataifa unasema watoto zaidi ya milioni saba wanahitaji msaada baada ya kutokea tetemeko la ardhi nchini Uturuki na Syria
Umoja wa mataifa unasema watoto zaidi ya milioni saba wanahitaji msaada baada ya kutokea tetemeko la ardhi nchini Uturuki na Syria REUTERS - REUTERS TV
Matangazo ya kibiashara

Kauli ya WHO imekuja saa chache tangu ujumbe wa kwanza wa umoja wa Mataifa, ufanikiwe kufika kwenye mji unaokaliwa na waasi, Aleppo, wakati huu taasisi hiyo ikikosolewa kwa kasi ndogo kuwasaidia waathirika wa tetemeko.

Hans Kluge, ni mkurugenzi wa WHO kanda ya Ulaya.

“Huu ni muda wa jamii ya kimataifa kuonyesha utu wake kwa nchi ya Uturuki kama ambavyo Uturuki imekuwa ikionyesha kwa mataifa mengine.” ameeleza Hans Kluge

Katika hatua nyingine, shirika la umoja wa Mataifa linalohudumia watoto UNICEF, limesema watoto zaidi ya milioni 7 wanahitaji msaada kufuatia madhara ya tetemeko hilo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.