Israel:Netanyahu anarejea madarakani kuongoza Israeli kwa miaka mitano
Benjamin Netanyahu, anarejea tena kama Waziri Mkuu wa Israeli baada ya kufanikiwa kuunda serikali.
Imechapishwa:
Cheza - 00:39
Netanyahu, mwenye umri wa miaka 73, anakuwa Waziri Mkuu wa muda mrefu nchini humo baada ya kuingia madaraka tangu mwaka 1996 hadi 1999 na baadaye, 2009 hadi 2021.
Nini kitarajiwe, kutoka kwa Netanyahu?
Dokta Brian Wanyama ni mchambuzi wa siasa za Kimataifa akiwa mjini Bungoma nchini Kenya.
“Raia wa Israeli wamempa nafasi ya pili, ya tatu na hata ya nne kuweza kuongoza taifa hilo na kumaanisha ya kwamba wanaimani katika utawala wake.” amesema Dkt Brian Wanyama.
Kinachosubiriwa sasa ni kuona jinsi ambavyo Netanyahu ataongoza taifa wakati huu dunia inapokabiliwa na kipindi kigumu cha uchumi na athari za Uviko 19.