ISRAEL-SIASA
Bunge la Israeli lavunjwa, uchaguzi mwingine kufanyika mwezi Novemba
Bunge nchini Israel limevunjwa ikiwa na maana kuwa taifa hilo sasa limeingia kwenye maandalizi ya uchaguzi mwingine, ambao utakuwa wa tano, chini ya miaka minne.
Imechapishwa:
Cheza - 00:31
Matangazo ya kibiashara
Waziri wa Mambo ya nje Yair Lapid anatarajiwa kukaimu nafasi ya Waziri Mkuu kunazia saa sita usiku, kuelekea uchaguzi huo utakaofanyika Novemba 1 na Waziri Mkuu wa zamani Benjamin Netanyahu anatarajiwa kuwania tena.
Je, ni kwanini imekuwa ni vigumu kwa Israeli kuwa na serikali thabiti ? Hamdun Marcel ni mchambuzi wa siasa za Kimataifa, anachambua hili akiwa jijini Mwanza, nchini Tanzania.