Pata taarifa kuu

Nyuklia: Tehran na Washington kufanya mazungumzo juu ya kuondolewa kwa vikwazo

Iran na Marekani zitaanza mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja "wiki hii" ambayo yatalenga "kuondoa vikwazo" vilivyowekwa na Washington. Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imetangaza.

Bendera ya Iran ikipepea huko Vienna, Austria, Mei 2021.
Bendera ya Iran ikipepea huko Vienna, Austria, Mei 2021. © AP Photo/Florian Schroetter, FILE
Matangazo ya kibiashara

"Nchi ya Ghuba ya Uajemi itakuwa mwenyeji wa mazungumzo na mkutano kati ya Iran na Marekani utakaofanyika wiki," msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Iran Saeed Khatibzadeh amesema wakati wa mkutano wa kila wiki.

Kauli hii inafuatia tangazo la Jumamosi la Umoja wa Ulaya na Iran la kuanza tena "katika siku zijazo" mazungumzo juu ya mpango wa nyuklia wa Iran - mazungumzo ambayo yaliyositishwa kwa zaidi ya miezi mitatu - Hayo yalibainishwa na mkuu wa diplomasia wa EU, Josep Borrell wakati wa ziara ya kushtukiza huko Tehran.

 Ili kuendeleza mchakato huo, Josep Borrell alionyesha kwamba mazungumzo "yasiyo ya moja kwa moja" kati ya Marekani na Iran yatafanyika haraka "katika nchi ya Ghuba".

"Tunachoenda kufanya katika siku zijazo hakihusu mwelekeo wa nyuklia, lakini tofauti zilizopo katika suala la kuondolewa kwa vikwazo," amesema Khatibzadeh.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.