YEMEN
Saudi Arabia kuwaachia huru wapiganaji wa Houthi
Jeshi la pamoja nchini Saudi Arabia, linaongoza vita dhidi ya wanajihadi wa kundi la Huthi la nchini Yemen, Limetangaza kuaachia huru baadhi ya wafungwa waasi wa kundi hilo.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Jeshi limesema kuwa limefanya haya kama njia moja ya kumaliza mapigano ya miaka saba sasa.
Wiki iliyopita, Jeshi hilo lilitangaza kuwa litawaachia huru wafungwa 163 waotuhumiwa kwa kuendeleza uhasama dhidi ya Saudi Arabia.
Mapigano kati ya pande hizi mbili yamesababisha vifo vya mamia ya elfu wa raia, ambapo pia Yemen imekumbwa na baa la njaa kutokana na machafuko haya.