Israeli kujenga nyumba mpya 1,355 katika Ukingo wa Magharibi
Kwa mara ya kwanza tangu kuundwa kwake, serikali ya Naftali Bennett inapinga wazi wazi Marekani kwa kutoa wito wa zabuni za ujenzi wa nyumba 1,355 katika Ukingo wa Magharibi.
Imechapishwa:
Nyumba hizi mpya 1,355 zitajengwa katika makazi saba katika Ukingo wa Magharibi. Jiji la Ariel, moja wapo ya makazi makubwa zaidi, peke yake litakuwa nyumba 729.
Wizara ya Ujenzi ya Israeli pia imebaini nia yake ya kuongeza mara mbili idadi ya Wayahudi wa Bonde la Yordani na mpango wa kuuza nyumba 1,500 katika eneo hili ifikapo mwaka 2026. "Kuongeza uwepo wa Wayahudi katika Ukingo wa Magharibi ni muhimu katika maono ya Wazayuni," ametangaza Zeev Elkin.
Siku ya Jumatano, kamati ya mipango ya Wizara ya Ulinzi ya Israeli inatarajiwa kutoa idhini ya mwisho kwa ujenzi wa nyumba zaidi ya 3,000 katika Ukingo wa Magharibi.