Pata taarifa kuu
LEBANON-UCHUNGUZI-USALAMA

Mlipuko Beirut: Rais wa Lebanon afutilia mbali uchunguzi wa kimataifa

Rais wa Lebanon Michel Aoun, ametupilia mbali uchunguzi wowote wa kimataifa kuhusu mlipuko mbaya uliyotokea katika bandari ya mjini Beirut, ambao uligharimu maisha ya zaidi ya watu 150, akibaini kwamba uchunguzi huo utapotosha ukweli.

Rais wa Lebanon Michel Aoun.
Rais wa Lebanon Michel Aoun. Dalati Nohra/Handout via REUTERS
Matangazo ya kibiashara

Rais wa Lebanon pia amesema ni muhimu kurejelea upya mfumo wa kisiasa "uliozorota", siku moja baada ya mwenzake wa Ufaransa, Emmanuel Macron, kuzuru nchi hiyo na kutoa wito kwa viongozi "kubadili mfumo" wa kisiasa nchini Lebanon.

"Tunatakiwa kurejelea upya mfumo wetu wa makubaliano, kwa sababu umezorota na hauruhusu kuchukuwa maamuzi ambayo yanaweza kutekelezwa kwa haraka: lazima kukubaliana na kupitia mamlaka kadhaa," rais Aoun amesema.

Siku ya Alhamisi waandamanaji wenye hasira walikabiliana na maafisa wa usalama jijini Beirut wakilaani mlipuko uliotokea katika ghala la kuhifadhi kemikali.

Waandamanaji wanailaumu serikali kwa utepetevu, suala ambalo wanaamini lilisabababisha mlipuko huo mkubwa na sasa wanataka uchunguzi wa kimataifa kufanyika.

Eneo la Tukio; Jengo hilo lilikuwa limehifadhi tani 2,750 ya kemikali ya ammonium nitrate.
Eneo la Tukio; Jengo hilo lilikuwa limehifadhi tani 2,750 ya kemikali ya ammonium nitrate. REUTERS/Mohamed Azakir TPX IMAGES OF THE DAY
Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.