Pata taarifa kuu
SYRIA-UFARANSA

Ufaransa yasema waasi wa Islamic State wataondolewa kabisa mjini Raqa

Muungano wa nchi za Magharibi unaopambana na kundi la Islamic State nchini Syria, unasema hivi karibuni wapiganaji hao wataondolewa kabisa kutoka katika ngome yao  kuu ya mji wa Raqa.

Mwanajihadi wa kundi la wapiganaji wa Dola la Kiislam katika mji wa Raqa nchini Syria, Septemba 16 mwaka 2014.
Mwanajihadi wa kundi la wapiganaji wa Dola la Kiislam katika mji wa Raqa nchini Syria, Septemba 16 mwaka 2014. AFP/STR
Matangazo ya kibiashara

Waziri wa Ulinzi wa Ufaransa Jean-Yves Le Drian amesema jeshi la muungano wa nchi hizo lipo tayari kwa makabiliano hayo.

"Leo, tunaweza kusema kuwa mji wa Raqa utashuhudia makabiliano makali hivi karibu,” amekiambia kituo cha Televisheni cha CNEWS.

Mji wa Raqa umekuwa ngome ya muda mrefu wa kundi la Islamic State nchini Syria pamoja na ile wa Mosul nchini Iraq.

Hata hivyo, Le Drian amesema makabiliano hayo yatakuwa magumu lakini ni lazima wapiganaji hao wakabiliwe.

Kundi la Islamic State nchini Syria pia limekuwa likishambuliwa na wanajeshi wa Urusi, nchi ambayo kwa sasa ni mshirika wa karibu wa rais Bashar Al Assad.

Wakati hayo yakijiri, mazungumzo ya amani kuhusu mzozo wa Syria yanaendelea jijini Geneva nchini Uswizi kati ya serikali ya Damascus na upinzani.

Mazungumzo haya yanaongozwa na Msuluhishi wa Umoja wa Mataifa Staffan de Mistura.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.