MAREKANI-SAUDI ARABIA
Barack Obama ziarani Saudi Arabia
Rais wa Marekani Barack Obama amewasili nchini Saudi Arabia kwa ziara ya siku mbili.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Obama anatarajiwa kutumia ziara hii kuonyesha ushirikiano wa nchi hiyo katika vita dhidi ya Wanajihadi.
Mzozo wa Syria na Yemen pia utajadiliwa katika ziara hiyo.
Baadhi ya wanasiasa nchini Marekani walishtumu ziara hii ya rais Obama wakiishtumu serikali ya Riyadh kwa kuhusika na shambulizi ya kigaidi mwaka 2001.
Rais Obama pia atahudhuria mkutano wa mataifa ya Ghuba.