Palestina yaiomba ICC kuchunguza uhalifu uliyotokea Gaza
Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wa Kivita ICC, yenye mako yake mjini Hague, Uholanzi, imeiponzgeza Palestina kwa uamzi iliyochukua.
Imechapishwa:
Mahakama hiyo ya Kimataifa ya Uhalifu wa Kivita ICC,imesema Mamlaka ya Palestina imetambua uwezo wake wa kuchunguza kuhusu uwezekano wa kutokea kwa visa vya ukiukwaji wa haki za binadamu katika eneo la Gaza mwaka uliopita.
ICC imesema inatambua kuwa ina jukumu la kuchunguza ikiwa wanajeshi wa Isreal walitekeleza uhalifu wakati wa Operesheni yao katika eneo hilo lakini Mahakama hiyo imeweka wazi kuwa kutambua huko hakumaanishi kuwa itaanza mara moja uchunguzi huo.
Palestina iliomba kuwa mwanachama wa Mahakama hiyo, ombi ambalo bado linatathminiwa na Umoja wa Mataifa.
Waziri Mkuu wa Israeli Benjamin Netanyahu amesema hatakubali wanajeshi wake kushatakiwa katika Mahakama hiyo ikiwa Palestina itakubaliwa kuwa mwanachama.