Wawili wauwawa, sita wajeruhiwa katika machafuko mapya nchini Syria
Raia wawili wa Lebanon wameuwawa na wengine sita wamejeruhiwa katika mji wa Kaskazini mwa Lebanon wa Tripoli , baada ya mapigano ya usiku wa manane jana Jumamosi huku kukiwa na mapigano ya madhehebu ya kidini yanayohusishwa na vita katika nchi jirani ya Syria, afisa usalama amesema.
Imechapishwa:
Mapigano hayo ya bunduki na roketi yaliibuka kati ya wakazi wa wilaya maskini ya Bab al- Tebbaneh na Jabal Mohsen, ambao wanaabudu katika madhehebu ya Sunni dhidi ya Alawites ambao ni jamii ya kidini ya rais wa Syria Bashar al-Assad.
Mauaji ya watu hao wawili wa Jabal Mohsen yalivunja utulivu ambao umekuwepo tangu Ijumaa asubuhi, wakati jeshi lilipopeleka askari katika maeneo ya eneo hilo la mji wa bandari.