Wakaazi wa EAC wanamatumaini mwaka wa 2023 utakuwa mwenye mafanikio
Msikilizaji wakati huu uchumi wa dunia ukitabiriwa kukua kwa kasi ndogo mwaka huu, wananchi kwenye nchi za Afrika Mashariki wamekuwa na maoni mseto, baadhi wakiamini hali itaimarika huku wengine wakihofia kutumbukia kwenye lindi la umasikini.
Imechapishwa:
Cheza - 00:37
Janga la uviko19, vita nchini Ukraine ni miongoni mwa mambo yaliyoteteresha uchumi w anchi za ukanda, lakini je nchi hizi zitarajie nini? Johnson Denge, ni mtaalamu wa masuala ya uchumi akiwa Nairobi, Kenya.
“Tuangalie kama kutakuwa na mabadiliko kwa vit aya Ukraine na Urusi ilikuwezesha mafuta kuwa bei nafuu kidogo.” Ameeleza Johnson Denge.
Raia wengi katika mataifa ya Afrika na hata katika sehemu zengine za dunia wameendelea kulalamikia mfuko wa be iza bidhaa, baadhi yao wakipoteza ajira kutokana na athari za uviko 19.