Pata taarifa kuu
JAMUHURI YA AFRIKA YA KATI-Joseph Kony kujisalimisha

Marekani yatilia mashaka uamuzi wa Kony kujisalimisha

Marekani imeingiwa mashaka juu ya taarifa ya kiongozi wa waasi wa LRA wa nchini Uganda kufanya mazungumzo ya kutaka kujisalimisha kwa madai kuwa baadhi ya waasi walishauriana na serikali ya Jamuhuri ya Afrika ya Kati na sio Kony kama ilivyosemekana.

Kiongozi wa waasi wa LRA Joseph Kony ataka kuhakikishiwa usalama wake ili ajisalimishe
Kiongozi wa waasi wa LRA Joseph Kony ataka kuhakikishiwa usalama wake ili ajisalimishe AFP PHOTO / OZAN KOSE
Matangazo ya kibiashara

Mapema alhamisi taarifa zilibainisha Serikali ya Jamuhuri ya Afrika ya kati CAR kujadiliana na kiongozi wa waasi na raia wa Uganda Joseph Kony kwa lengo la kujisalimisha.

Kwa mujibu wa msemaji wa serikali ya jamuhuri ya kati, Joseph Kony ametaka kuhakikishiwa usalama wake kabla hajajisalimisha.

Kony,ambaye ni kiongozi wa waasi wa LRA anatafutwa na mahakama ya uhalifu wa kivita anakokabiliwa na kesi ya uhalifu wa kivita.

Serikali ya Marekani iliahidi kutoa kitita cha dola za Marekani milioni 5 kwa atakayefanikisha kupatikana kwa Joseph Kony.

Hii ni kwa mara ya kwanza Joseph Kony anapatikana tangu miaka kadhaa kupita.

Siku ya jumatano mjumbe maalumu wa umoja wa Afrika Francisco Madeira, alibainisha kuwa baraza la usalama la Umoja wa Mataifa limeona ripoti kuwa Joseph Kony anaugua sana ugonjwa ambao haujaweza kufahamika.

Mnamo mwezi April Jeshi la Uganda lilisitisha harakati za kumsaka Kony huko jamuhuri ya Afrika ya kati wakilaumu kufanyiwa ukatili na serikali ya waasi iliyokuwa ikidhibiti huko.

Joseph Kony na wapiganaji wanaokadiriwa kufikia 200-500 wa kundi la waasi wa Lord's Resistance Army (LRA) limesababisha mapigano nchini Uganda na ukanda huo kwa zaidi ya miongo miwili.

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.