UBELGIJI
Viongozi wa umoja wa Ulaya EU kukutana baadaye hii leo jijini Brussels
Ma rais na serikali za nchi za Umoja wa Ulaya EU wanataraji kukutana leo jioni kwenye makao makuu ya Umoja huo jijini Brusels Ubelgiji ili kujaribu kutafuta muafaka kuhusu muswada wa bajeti ya umoja wa Ulaya kwa kipindi cha mwaka 2014-2020.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Mkutano huo utatanguliwa na ule wa viongozi wa vyama vya European social democrats ambao utawakutanisha Kansela Angela Merkel na rais Francois Hollande mapema majira ya mchana kabla ya mkutano huo wa umoja wa Ulaya chanzo kimoja kimeeleza.
Aidha chanzo hicho kimebainisha kuwa viongozi hao watamteua Yves Mersch kuwa mkurugenzi mkuu wa Benki kuu ya Ulaya.