Pata taarifa kuu
MALAWI

Malawi yajivua wenyeji wa mkutano wa Umoja wa Afrika AU

Malawi imetangaza kuahirisha kuwa mwenyeji wa mkutano wa kilelel wa umoja wa Afrika uliopangwa kufanyika mwezi ujao nchini humo,kufuatia mzozo baina yake na umoja wa Afrika ambao unasisitiza kumualika rais wa Sudani Omar Al Bashir ambaye anatakiwa na mahakama ya uhalifu wa kivita ICC.

Rais wa Malawi Joyce Banda ambaye ametangaza nchi yake kujivua wenyeji wa mkutano wa AU
Rais wa Malawi Joyce Banda ambaye ametangaza nchi yake kujivua wenyeji wa mkutano wa AU Reuters
Matangazo ya kibiashara

Makamu wa Rais Khumbo Kachali amesema kuwa serikali imekataa kuwapigia magoti wanachama 54 wa Umoja wa Afrika kuhusu rais Bashir, ambaye anatafutwa na mahakama ya uhalifu wa kivita ICC kwa tuhuma za mauaji ya kimbari, uhalifu dhidi ya binadamu na uhalifu wa kivita,kuhudhuria mkutano wa Lilongwe.

Mapema siku ya Alhamisi, Sudan ilitoa wito kwa umoja wa Afrika AU kuhamisha mkutano huo kutoka Liongwe Malawi na ufanyikie kwenye makao makuu yake mjini Addis Ababa Ethiopia baada ya Malawi kutangaza kuwa rais Bashir hakaribishwi nchini humo.

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.