YEMEN
Wanajeshi 9 wa Yemen wauwawa na wapiganaji wa Al Qaeda
Wanajeshi tisa wa Yemen wameuwawa na wapiganaji wa kundi la Al Queda katika jaribio la kuteka kituo cha jeshi lililofanywa na wapiganaji hao katika jimbo la Abyan na kusababisha vurugu na majibishano ya risasi.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Taarifa za maafisa katika jimbo hilo zimethibitisha kuuwawa kwa wanajeshi hao tisa na kuongeza kuwa wanajeshi wengine kadhaa wamekamatwa.
Aidha wanajeshi waliojeruhiwa wengiwao wakiwa na sare za jeshi wamepelekwa katika hospitali ya kijeshi ya Bashib ambako wanapatiwa matibabu .
Hata hivyo taarifa zaidi zinaeleza kuwa wanajeshi wengine waliojeruhiwa bado hawajaondolewa katika eneo hilo.