SYRIA
Jumuiya ya nchi za kiarabu yasitisha Operesheni yake nchini Syria.
Jumuiya ya nchi za kiarabu imesema inasitisha operesheni ya waangalizi wake nchi Syria kufuatia kuongezeka kwa machafuko nchini humo.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Mkuu wa ujumbe wa waangalizi hao nchini Syria Ahmed Mustafa al Dabi amesema kuwa machafuko yanayoendelea hayasaidii kuzileta pande zote mbili katika meza ya mazungumzo.
Hatua ya kusitishwa kawa operesheni hiyo inakuja siku moja baada ya taarifa ya kiongozi huyo kubainisha kuwa machafuko yameongezeka zaidi juma hili hasa katika miji ya Homs, Hama na Idlib.
Taarifa rasmi kuhusu uamuzi huo zitatolewa hapo baadaye.