SYRIA
Mauaji yaendelea nchini Syria licha ya kuwepo kwa waangalizi.
Wakati viongozi mbalimbali wa dini duniani wakitoa wito wa kusitishwa kwa vurugu nchini syria, kumeripotiwa mauaji ya watu kadhaa kwenye mji wa Homs huku mkuu wa timu ya waangalizi toka Umoja wa kiarabu akiagiza kuelekea haraka kwa waangalizi kwenye mji huo.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Wanaharakati katika mji huo wamesema kuwa kuwa usiku wa kucha milio ya risasi imeendelea kusikika katika kila kona za mji huo huku wakieleza kuwa zaidi ya askari elfu nne wa nchi hiyo wameingia kwenye mji huo.