SYRIA
Watu kumi na saba wameuwawa katika maandamano nchini Syria.
Takribani watu kumi na saba wameuwawa na wanajeshi wa serikali nchini Syria wakati wa maandamno kuishinikiza jumuiya ya nchi za kiarabu kuiadhibu serikali ya rais Bashar Al Assad.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Wanaharakati wa upinzani wamesema kuwa zaidi ya waandamanaji laki mbili walikutana katika mji wa Homs pekee hapo jana ambako watu tisa wameripotiwa kuuwa.
Watu wengine watatu wameripotiwa kuuwawa katika mji wa Hama,na wengine watatu wameuwawa katika jimbo la Deraa na wawili katika maeneo ya mji wa Damascus.