Norway
Anders Behring Breivik kusikilizwa kesho na polisi
Polisi nchini Norway wanasema kuwa, kesho Ijumaa watamhoji Anders Behring Breivik mwanaume mwenye umri wa miaka 32 aliyekiri kuwauawa watu 76 juma lililopita kwa kuwapiga risasi na kutekeleza shambulizi la bomu jijini Oslo.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Matangazo ya kibiashara
Polisi wanasema kuwa wametamatisha uchunguzi wa kuwasaka watu wengine wanaosemekana kupotea katika kisiwa cha Utoeya, eneo la mkasa huo.
Waziri Mkuu wa Norway,Jens Stoltenberg anasema serikali yake haitatishwa na shambulizi hilo na anaamini kuwa uchunguzi utabaini mengi zaidi kuhusu mauaji hayo.