Pata taarifa kuu

Putin aishtumu Marekani kwa kujaribu kuingiza urusi kwenye vita

Rais wa Urusi Vladimir Putin ameishtumu Marekani kwa kuendelea kuichochea nchi yake kuingia kwenye vita na Ukraine, kwa kile alichokieleza Washington inatafuta mbinu za kuiwekea Moscow vikwazo.

Rais wa Urusi Vladimir Putin alipokuwa akihutubia wanahabari wakati wa mkutano wa pamoja na Waziri Mkuu wa Hungary Viktor Orban kufuatia mazungumzo yao katika Ikulu ya Kremlin mjini Moscow Jumanne, Februari 1, 2022.
Rais wa Urusi Vladimir Putin alipokuwa akihutubia wanahabari wakati wa mkutano wa pamoja na Waziri Mkuu wa Hungary Viktor Orban kufuatia mazungumzo yao katika Ikulu ya Kremlin mjini Moscow Jumanne, Februari 1, 2022. AP - Yuri Kochetkov
Matangazo ya kibiashara

Aidha, ameilamu Marekani kwa kupuuza malalamishi yake ya kiusalama, iwapo Ukraine itaruhusiwa kuwa mwanachama wa Jeshi ya kujihami la nchi za Magharibi NATO.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu wa Uingereza Bori Johnson ambaye amezuru Ukraine, amesema nchi yake na mataifa mengine ya Magharibi yako tayari kuichukulia Urusi hatua iwapo itaendelea na mpango wake.

Hali ya wasiwasi imeendelea kushuhudiwa wakati huu, maelfu ya wanajeshi wa Urusi wakiendelea na mazoezi katika mpaka na Ukraine.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.