Coronavirus: Taiwan yadai China imezuia mkataba na BioNTech
Taiwan imeshutumu moja kwa moja China kwa kuzuia mkataba ambao ilikuwa imefanya na maabara ya BioNTech kupata dozi ya chanjo yake ya COVID-19.
Imechapishwa:
Taiwan imeagiza dozi Milioni kadhaa za chanjo kutoka maabara ya AstraZeneca na Moderna, lakini hadi sasa imepokea zaidi ya dozi 700,000, ikilinda tu 1% ya raia wake licha ya kuzuka tena kwa virusi.
"Tulikuwa karibu kumaliza mkataba na kiwanda asili cha Ujerumani (cha BioNTech), lakini kwa sababu ya kuingiliwa kati na China, hadi sasa hatujaweza kufikia mkataba huo," amesema Rais wa nchi hiyo Tsai Ing-wen wakati wa mkutano wa Chama kinachoongoza katika eneo hilo.
Ikiwa BioNTech imekataa kutoa maoni juu ya matamshi ya Tsai Ing-wen, maabara hiyoya Ujerumani imeongeza, hata hivyo, kwamba inaunga mkono usambazaji wa chanjo duniani.