Pata taarifa kuu
MYANMAR

Mapinduzi Myanmar: Polisi yakabiliana na waandamanaji Naypyidaw

Vikosi vya usalama vimetumia maji kujaribu kuzima maandamno ya waandamanaji wanaopinga mapinduzi ya kijeshi huko Naypyidaw, mji mkuu wa Burma leo Jumanne, kulingana na picha zilizorushwa moja kwa moja kwenye runinga.

Kiongozi wa kiraia wa Myanmar, Aung San Suu Kyi,
Kiongozi wa kiraia wa Myanmar, Aung San Suu Kyi, Thet Aung / AFP
Matangazo ya kibiashara

Kundi hili dogo la waandamanaji lilikataa kutawanyika mbele ya kizuizi cha polisi, huku wakipiga kelele na kusema "acheni udikteta wa kijeshi".

Maandamano haya yameingia kwa siku ya nne mfululizo leo Jumanne. Waandamanaji wanaendelea kuomba kiongozi wa chama cha LND Aung San Suu Kyi na viongozi wengine wa chama hiki waachiliwe huru mara moja

Siku ya Jumapili, maandamano, makubwa zaidi tangu maandamano kiraia ya mwaka 2007 yaliyokandamizwa vibaya na jeshi, yalifanyika bila kusababisha hasara kubwa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.