Pata taarifa kuu
MYANMAR-ICJ-HAKI

Kiongozi wa Myanmar aonya majaji wa ICJ kutoruhusu kuendelea kwa kesi dhidi ya nchi yake

Kiongozi wa Myanmar Aung San Suu Kyi amewataka majaji kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Haki kutupilia mbali kesi ya mauaji ya kimbari dhidi ya nchi yake.

Aung San Suu Kyi mbele ya  Mahakama ya Kimataifa ya Haki, ICJ, Hague ambapo Burma inashtakiwa kwa mauaji ya kimbari, Desemba 11, 2019.
Aung San Suu Kyi mbele ya Mahakama ya Kimataifa ya Haki, ICJ, Hague ambapo Burma inashtakiwa kwa mauaji ya kimbari, Desemba 11, 2019. REUTERS/Yves Herman
Matangazo ya kibiashara

Kiongozi huyo ameonya kuwa kuendelea kwa kesi hiyo kutachochea mzozo zaidi ambao mpaka sasa umesababisha karibu robo milioni ya waislamu jamii ya Rohingya kukimbia nchi hiyo.

Akihitimisha utetezi wake mbele ya mahakama hiyo, Aung San Suu Kyi alitoa onyo kali kwa majaji ikiwa wataruhusu kuendelea kwa kesi iliyowasilishwa na nchi ya Gambia dhidi ya Myanmar, akisema itadumaza mchakato wa maridhiano.

Suu Kyi ambaye wakati mmoja alikuwa muhanga wa vitendo vya unyanyasaji wa wanajeshi wa nchi hiyo na kumfanya ashinde tuzo ya amani ya Nobel, ndio amekuwa mstari wa mbele safari hii kuwatetea kwa makosa waliyotekeleza dhidi ya jamii ya Rohingya nchini Mwake.

Mashirika ya kutetea haki za binadamu na hata wajumbe wa kamati ya tuzo ya amani ya Nobel, sasa wanataka tuzo aliyopewa kiongozi huyo ifutwe na achukuliwe kama mmoja wa watu wanaoshiriki kuwaficha wahalifu wa vitendo vya ukatili dhidi ya binadamu.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.