Wanajeshi 8 wa Pakistan wauawa katika shambulio la wanamgambo wa Taliban
Wanajeshi saba wa jeshi la Pakistan wameripotiwa kuuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa vibaya katika shambulio lililotekelezwa na wanamgambo wa kundi la Taliban jimboni Shidano Dand.
Imechapishwa:
Wanamgambo wa Taliban walitekeleza shambulio hilo usiku wa kuamkia leo katika kituo cha ukaguzu kaskazini mwa nchi hizo kwenye mji wa Kurrama na kuwashambulia askari waliokuwa doria na kuwaua wanajeshi saba.
Kwa mujibu wa msemaji wa Jeshi la Pakistan, amesema kuwa mbali na kupoteza wanajeshi saba lakini jeshi lake limefanikiwa kuwaua wanamgambo zaidi ya kumi na nane baada ya kutokea makabiliano ya risasi kati yao.
Eneo hilo ambalo ndilo ngome za wapiganaji wa Al-Qaeda na wanamgambo wa Taliban limekuwa kama ndio kitovu cha mashambulizi dhidi ya wanajeshi wa serikali katika vituo vingi vya ukaguzi vinavyosimamiwa na wanajeshi wa Pakistan.
Shambulio hilo limekuja ikiwa zimepita siku mbili tu, toka wanamgambo hao wafanye shambulio la kushtukiza kwenye eneo hilohilo na kuua wanajeshi nane wa Pakistan.