Pakistani-Marekani
Pakistani yaendelea kukaidi amri ya Marekani ya kutaka iangamize ,kundi la Haqqani
Serikali ya Pakistan imeendelea kukaidi amri ya Marekani ambayo inaitaka nchi hiyo kuchukua hatua za haraka kuuangamiza Mtandao wa Haqqani ambao unatuhumiwa kufanya mashambulizi ya Ubalozi wa Marekani nchini Afghanistan.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Mkutano wa pamoja wa kusaka umoja baina ya Waziri Mkuu Yousuf Raza Gilani, viongozi wa vyama vya upinzani, viongozi wa dini pamoja na Makamanda wa Kijeshi umefikia uamuzi wa kupuuzia mbali shinikizo la Marekani.
Waziri Mkuu Gillani amekiri nchi yake imeshtulia mno na kauli ya Marekani ambayo inaitaka nchi hiyo kuuangamiza Mtandao wa Haqqani kwa kisingizio cha kupambana na ugaidi katika taifa hilo.