Pata taarifa kuu
Pakistani-Marekani

Pakistani yaendelea kukaidi amri ya Marekani ya kutaka iangamize ,kundi la Haqqani

Serikali ya Pakistan imeendelea kukaidi amri ya Marekani ambayo inaitaka nchi hiyo kuchukua hatua za haraka kuuangamiza Mtandao wa Haqqani ambao unatuhumiwa kufanya mashambulizi ya Ubalozi wa Marekani nchini Afghanistan.

Jeshi la Pakistani likiwatia nguvuni washukiwa kadhaa wa mashambulizi
Jeshi la Pakistani likiwatia nguvuni washukiwa kadhaa wa mashambulizi Reuters/Athar Hussain
Matangazo ya kibiashara

Mkutano wa pamoja wa kusaka umoja baina ya Waziri Mkuu Yousuf Raza Gilani, viongozi wa vyama vya upinzani, viongozi wa dini pamoja na Makamanda wa Kijeshi umefikia uamuzi wa kupuuzia mbali shinikizo la Marekani.

Waziri Mkuu Gillani amekiri nchi yake imeshtulia mno na kauli ya Marekani ambayo inaitaka nchi hiyo kuuangamiza Mtandao wa Haqqani kwa kisingizio cha kupambana na ugaidi katika taifa hilo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.