Pata taarifa kuu

Watu 17 wameripotiwa kuuawa katika shambulio Sudan Kusini

Nairobi – Watu 17 wameripotiwa kuuawa nchini Sudan Kusini kwenye jimbo la Jonglei, baada ya vijana waliokuwa na silaha kutoka Duk kushambulia raia. Aidha vijana hao wanadaiwa kuiba zaidi ya ng’ombe elfu saba.

Watu 17 wameripotiwa kuuawa nchini Sudan Kusini kwenye jimbo la Jonglei
Watu 17 wameripotiwa kuuawa nchini Sudan Kusini kwenye jimbo la Jonglei AFP
Matangazo ya kibiashara

Mapigano haya yamethibitishwa na Peter Lajor Duk kamishena wa kaunti ya Duk, jimboni Jonglei.

Mapigano makali yalizuka kwenye kaunti ya Duk, mapigano hayo yalisababisha vifo na watu 17 kujeruhiwa.”alisemaPeter Lajor Duk.

00:14

Peter Lajor Duk kuhusu Jonglei

Aidha viongozi wa Jonglei, wamelaani mashambulio hayo, wakitaka idara za usalama kuingilia kati, Elizabeth Nyaban anaeleza.

Waliotekeleza mashambulio hayo ni vijana.” alieleza Elizabeth Nyaban.

00:04

Elizabeth Nyaban

Tukio hili linahusishwa na hatua ya vijana wengi kwenye eneo la Pibor kumiliki bunduki kiholela, kama anavyoeleza Abraham Kelang, waziri wa habari wa jimbo hilo.

Vijana wengi wana bunduki. Ripoti tunayopata si nzuri.  Hata hivyo tunalaani vikali kitendo chao cha uhalifu.” alieleza Abraham Kelang.

00:14

Peter Lajor Duk kuhusu Jonglei

Majimbo ya Jonglei na Pibor, yamekuwa na utata wa zaidi ya miaka kumi ambako watu wa kabila la Murle hupigana na watu wa kabila la Nuer. Makabila yote ni ya watu wafugaji. Mara kwa mara mapigano yao yanatokana na wizi wa mifugo

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.