Pata taarifa kuu

Senegal: Ousmane Sonko kujua hatma yake kuwania urais mwakani

NAIROBI – Mahakama nchini Senegal inatarajiwa kufanya uamuzi hii leo kuhusu hatima ya  kiongozi wa upinzani Ousmane Sonko aliyeondolewa kwenye orodha ya wagombea Urais kufuatia uchaguzi wa mapema mwaka ujao.

Mpinzani nchini Senegal Ousmane Sonko huko Dakar mnamo Machi 2021.
Mpinzani nchini Senegal Ousmane Sonko huko Dakar mnamo Machi 2021. AP - Sylvain Cherkaoui
Matangazo ya kibiashara

Hii leo mahakama ya Dakar nchini Senegal itaamua endapo kiongozi wa upinzani, Ousmane Sonko, anapaswa kurudishwa katika daftari la uchaguzi, hatua ambayo itaamua kuhusu hatima yake ya kugombea uchaguzi ujao wa rais.

Kiongozi huyo wa upinzani aliondolewa kwenye daftari la uchaguzi baada ya kuhukumiwa kifungo cha miaka miwili jela mwezi Juni baada ya kupatikana na hatia ya kuwapotosha vijana kimaadili.

Mwanasiasa huyo amekuwa katikati ya mvutano na serikali kwa kipindi cha zaidi ya miaka miwili, hali iliyozusha machafuko mara kadhaa nchini Senegal.

Sonko anadai kesi zinazomuandama zimeundwa, kwa lengo la  kumzuia kugombea uchaguzi wa rais,madai ambayo serikali imeyakanusha ikisema haina ushawishi katika mfumo wa mahakama.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.