Pata taarifa kuu

EAC: Ufadhili wapungua mabadiliko ya hali ya hewa yakiendelea kushuhudiwa

Nairobi – Misaada ya kibinadamu imeonekana kuaanza kupungua katika baadhi ya nchi za Afrika Mashariki wakati huu zinapokabiliwa na mafuriko yanayosababishwa na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha, karibia watu 130 katika nchi za Ethiopia, Kenya na Somalia.

Idara ya utabiri wa hali ya hewa nchini Kenya imeonya kuwa mvua inayoshuhudiwa itaendelea hadi mwezi Januari mwaka wa 2024
Idara ya utabiri wa hali ya hewa nchini Kenya imeonya kuwa mvua inayoshuhudiwa itaendelea hadi mwezi Januari mwaka wa 2024 AP - Stringer
Matangazo ya kibiashara

Mataifa yalio kwenye pembe ya Afrika ndiyo yameathirika zaidi na mafuriko hayo yanayoshuhudiwa baada ya kukabiliwa na ukame wa muda mrefu zaidi katika kipindi cha miaka 40.

Licha ya kuwepo kwa uhitaji mkubwa wa misaada ya kibindamu katika nchi hizo tatu za Kenya, Somalia na Ethiopia, misaada hiyo imeripotiwa kupungua kwa Dolla bilioni 4.1 tangu mwazoni mwa mwaka huu peke.

Watu zaidi ya 50 wameripotiwa kufariki katika mafuriko nchini Kenya
Watu zaidi ya 50 wameripotiwa kufariki katika mafuriko nchini Kenya © Kelvin Ogome / RFI

Inahofiwa kuwa huenda hali ikawa mbaya zaidi haswa wakati huu wahisani kama vile Uingereza, Canada na Ujerumani zikipanga kupunguza ufadhili wake mwaka ujao kwa asilimia 50.

Kwa mujibu wa ripoti ya shirika la misaada la Oxfam, mataifa tajiri duniani yalilipa chini ya asilimia tano peke ya Dolla bilioni 53.3 kwa mataifa ya Afrika Mashariki kukabiliana na changamoto zinazotokana na mabadiliko ya hali ya hewa.

Kaunti ya Mombasa nchini Kenya ni mojawapo ya maeneo yalioathirika zaidi ya mafuriko yanayotokana na mvua inayoendelea kunyesha kwenye taifa hilo
Kaunti ya Mombasa nchini Kenya ni mojawapo ya maeneo yalioathirika zaidi ya mafuriko yanayotokana na mvua inayoendelea kunyesha kwenye taifa hilo REUTERS - STRINGER

Kwa sasa mataifa ya Kenya, Somalia na Ethiopia yanahitaji bilioni saba kwa pamoja ilikuwasaidia waathiriwa wa mabadiliko ya hali ya hewa japokuwa ni asilimia 41 peke ya ufadhili ambayo imepatikana.

Nchini Somalia, zaidi ya watu milioni moja wameathirika na mafuriko baada ya mto Juba na Shabelle kuvunja kingo zake na kuharibu makazi yao.

Somalia ni mojawapo ya mataifa yalioathirika na mafuriko
Somalia ni mojawapo ya mataifa yalioathirika na mafuriko REUTERS - FEISAL OMAR

Haya yanajiri wakati huu mafuriko yakiwa yamesababisha vifo vya watu 52 nchini Kenya, familia zaidi elfu 15 zikipoteza makazi yao, hali sawia ikiripotiwa nchini Ethiopia.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.