Kongamano kuhusu afya ya umma la mwaka huu CPHIA 2023 linafanyika jijini Lusaka
Nairobi – Mkutano wa kila mwaka wa kimataifa wa afya ya umma barani Afrika (CPHIA) linaandaliwa na kituo cha Afrika cha kudhibiti na kuzuia magonjwa (Africa CDC) na hutoa nafasi ya kipekee kwa raia wa bara Afriaka pamoja na viongozi kutoka kwenye maeneo tofauti kutafakari mafunzo waliyopata katika afya na sayansi pamoja na kupanga namna ya kuunda mifumo thabiti zaidi ya afya.
Imechapishwa:
CPHIA 2023 ni kikao cha tatu kinachojiri baada ya mkutano uliofanyika kwa njia ya video mnamo mwaka wa 2021 na mwengine uliowakutanisha washika dau katika sekta ya afya jijini Kigali, Rwanda, mnamo 2022.
Mwaka huu, wizara ya afya nchini Zambia ndio itakuwa mwenyeji wa CPHIA 2023 mwezi huu wa Novemba kati ya tarehe 27-30 katika jiji la Lusaka.
Be part of the solution at #CPHIA2023 as we help chart a new path forward for African public health.
— CPHIA Official (@CPHIA_AfricaCDC) November 6, 2023
📆 Nov 27-30, 2023
📍 Lusaka, Zambia
🌐 “Breaking Barriers: Repositioning Africa in the global health architecture.”
To register, visit 👉🏾 https://t.co/Xcl0R1TeCO https://t.co/nkoAKTN5zn
CPHIA 2023 itafanyika ana kwa ana mjini Lusaka, Zambia katika barabara ya Kenneth Kaunda katika kituo cha mikutano cha kimataifa cha Mulungushi.
Iwapo unataka kujisajili unaweza kutembelea wavuti wa Cphia2023 kwa maelezo zaidi.Kwa kuzingatia maazimio ya mwaka uliopita, CPHIA 2023 inalenga kuonyesha namna bara la Afrika lilivyokabiliana na kuondoa vizuizi pamoja na kudhibitisha tena Afrika kama kituo chenye uwezo katika sayansi na uvumbuzi.
Kongamano hilo pia linatarajiwa kutoa nafasi kwa vijana wa bara Afrika.
The 2nd @AfricaCDC Youth Pre-Conference - #YPC2023 will feature panel sessions, presentations, workshops, and network sessions aimed at building the capacity of young public health professionals in Africa.
— African Union Bingwa Initiative (@AUBingwa) November 4, 2023
📍Lusaka, Zambia
📅November 25-26, 2023.#YouthLeadershipInHealth pic.twitter.com/poFrIoD6Lb
Aidha kikao cha mwaka huu kinalenga kuonyesha jinsi Afrika inauwezo wa kuzindua maarifa mapya na bidhaa za afya pamoja na kuwa kielelezo cha maendeleo.
Mkutano wa mwaka huu unakuja wakati huu mataifa ya Afrika yakiwa mbioni kujiweka sawa katika sekta ya afya ya umma haswa baada ya mlipuko wa uviko 19 ambapo sasa CPHIA inalenga kusaidia kujenga Afrika yenye mifumo bora ya afya, yenye ustawi zaidi katika ukanda wa Afrika na kidunia.
#CPHIA2023 is just 3 WEEKS away! Have you registered? Don't miss your opportunity to attend Africa's leading health conference. https://t.co/wMbJCkTjJP
— CPHIA Official (@CPHIA_AfricaCDC) November 6, 2023
Malengo ya kongamno la mwaka huu CPHIA2023:
Utayari wa kukabiliana na majanga pamoja na mikakati ya ufadhili kwa bara Afrika.
Kuimarisha na kuinua ubunifu wa bara Afrika pamoja na kuendeleza uzalishaji wa chanjo za ndani ya bara, uchunguzi wa magonjwa na upatikanaji wa tiba.
Kutoa nafasi ya upatikanaji wa afya kwa wote katika bara Afrika, kutilia nguvu usawa katika mifumo ya kiafya kwenye bara.
Upatikanji wa afya ya kutosha kwa wanawake, wasichana na wanawake wachanga barani Afrika.
Kubadilisha sekta ya afya barani Afrika kwa kutumia uvumbuzi wa kidigitali.
Kukabiliana na magonjwa ya kuambukizana barani Afrika pamoja na kushugulikia suala la afya ya akili.