Pata taarifa kuu

Mamlaka ya Niger imeanza kuwageukia washirika wapya baada ya mapinduzi

Nairobi – Miezi miwili na nusu baada ya kufanyika kwa  mapinduzi ya kijeshi nchini Niger mnamo Julai 26, dhidi ya Rais Mohamed Bazoum, nchi hiyo sasa imeanza kugeukia washirika wapya, baada ya kukabiliwa na vikwazo vya nchi wanachama wa Jumuiya ya Kiuchumi ya Afrika Magharibi, Ecowas.

Mamlaka ya Niger imeanza kuwageukia washirika wapya baada ya mapinduzi
Mamlaka ya Niger imeanza kuwageukia washirika wapya baada ya mapinduzi AP - Sam Mednick
Matangazo ya kibiashara

Utawala wa kijeshi jijini Niamey umesema licha ya kukatiwa misaada ya kibinadamu, ya kifedha kutoka taasisi mbali mbali za kimataifa, na kusitishwa kwa ushirikiano na mataifa ya magharibi miongoni mwao Ufaransa, lakini pia Marekani, na Umoja wa Mataifa, lakini bado kuna uwezekano wa kuwapata washirika wapya, Taarifa ya ikulu ya rais jijini Niamey imesema.

Wadadisi wa mambo wanasema tukio la hivi punde la kumfukuza mratibu wa Umoja wa Mataifa nchini Niger Luiza Aubin, kuondolewa kwa wanajeshi wa Ufaransa, na kusitishwa kwa baadhi ya ufadhili wa kimataifa huenda yakachangia kwa nchi hiyo kutumbukia katika lindi refu la umasikini.

Mohamed Bazoum alikuwa mshirika wa karibu wa Ufaransa na harakati zake katika ukanda wa Sahel
Mohamed Bazoum alikuwa mshirika wa karibu wa Ufaransa na harakati zake katika ukanda wa Sahel AFP - ISSOUF SANOGO

Utawala wa kijeshi nchini Niger umeshutumu kile unachokiita  ujanja" unaofanywa na katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, chini ya ushawishi wa Ufaransa", ili kuidhuru nchi yao.

Siku ya Jumanne, Marekani ilitangaza kuondoa msaada wa kiasi cha dola milioni 500 ili kufadhili miradi ya maendeleo, Hali ambayo huenda ikaathiri pakubwa juhudi za maendeleo ya kiuchumi ya nchi hiyo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.