Pata taarifa kuu

Liberia: Zoezi la kuhesabu kura limeanza

Nairobi – Shughuli ya kuhesabu kura inaendelea nchini Liberia baada ya kumalizika kwa zoezi la upigaji kura, kumchagua rais mpya na wabunge  siku ya Jumanne.

Zoezi la kuhesabu kura limeanza nchini Liberia
Zoezi la kuhesabu kura limeanza nchini Liberia REUTERS - CARIELLE DOE
Matangazo ya kibiashara

Raia katika taifa hilo la Afrika Magharibi walipiga kura kumchagua rais, wajumbe wa baraza la wawakilishi na baadhi ya wabunge wa Seneti.Rais aliye madarakani na mwanasoka wa zamani George Weah, ambaye anawania muhula wa pili, ndiye anayepigiwa upatu kuibuka mshindi.

Raia wa Liberia walipiga hapo jana Jumanne kuwachagua viongozi wao wapya
Raia wa Liberia walipiga hapo jana Jumanne kuwachagua viongozi wao wapya REUTERS - CARIELLE DOE

Weah, anakabiliwa na upinzani kutoka kwa wagombea wengine 19.

Makamu wa rais wa zamani Joseph Boakai na mfanyibiashara Alexander Cummings, ametajwa kuwa  mpinzani mkuu wa rais Weah.

Hali ya wasiwasi ilishuhudiwa wakati wa kipindi cha kampeni, vurugu zikishuhudiwa katika jimbo la Lofa kati wa wafuasi wa rais anayeondoka madarakani na wafuasi wa upinzani.

Rais Weah anawania kuongoza taifa hilo kwa muhula wa pili
Rais Weah anawania kuongoza taifa hilo kwa muhula wa pili REUTERS - CARIELLE DOE

Weah aliingia mdarakani mwaka wa 2017 baada ya majaribio mawili ya hapo awali kutofanikiwa.

Tume ya uchaguzi inatarajiwa kuanza kuchapisha matokeo ya kwanza leo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.