Pata taarifa kuu

Hali ya demokrasia nchini Sudan inaendelea kuyumba

Nairobi – Dunia inaadimisha siku ya Demokrasia  wakati huu hali demokrasia nchini Sudan ikiendelea kuyumba baada ya jeshi kumuondoa rais wa muda mrefu madarakani Omar al Bashir, mwaka 2019.

Jeshi la Sudan limekuwa likikabiliana na wapiganaji wa RSF hali inayotishia kuyumbisha zaidi demokrasia nchini humo
Jeshi la Sudan limekuwa likikabiliana na wapiganaji wa RSF hali inayotishia kuyumbisha zaidi demokrasia nchini humo © AFP
Matangazo ya kibiashara

Matumaini ya wananchi wa Sudan, kuongozwa kidemokrasia, yameendelea kudidimia baada ya vita kuzuka kati ya jeshi na wapiganaji wa RSF tangu Aprili 15.

Mpaka sasa jitihada za Kimataifa na kikanda kujaribu kurejesha hali ya kidemokrasia na kukomesha vita, hazijazaa matunda.

Makabiliano yamekuwa yakiendelea  nchini Sudan licha ya Pande hasimu kutakiwa kusitisha mapigano
Makabiliano yamekuwa yakiendelea nchini Sudan licha ya Pande hasimu kutakiwa kusitisha mapigano © AP

Hassan Khannenje ni mtafiti wa masuala ya kikanda kutoka Shirika la Horn, anathmini kinachoendelea nchini Sudan akiwa jijini Nairobi.

Inaonekana kuwa wanaopigana Khartoum wana imani na wakuu wa nchi jirani ya Sudan Kusini, kutatua na kumaliza mapigano, Sudan ilisaidia kwa kiwango kikubwa katika mchakato wa kurejesha amani Sudan kusini, Ni dhahiri kuwa Sudan iko tayari kukaribisha Sudan kusini katika juhudi za kumaliza mapigano yanayoendelea. ” alisema Hassan Khannenje ni mtafiti wa masuala ya kikanda kutoka Shirika la Horn.

00:12

Hassan Khannenje ni mtafiti wa masuala ya kikanda kutoka Shirika la Horn

Mchambuzi wa siasa za Kimataifa na uhusiano wa Kimataifa Profesa Macharia Munene, anasema Sudan ina safari ndefu kupata demokrasia thabiti.

Wakati uhuru umetoweka popote, kutoweka kwa uhuru huo unamaanisha utumwa. Una maana kuwa nchi haizwei kufikiriwa kuwa huru. Kwa njia nyingine kuwepo kwa demokrasia ni kuwa huru. Kukosekana kwa uhuru ni kutoweka kwa demokrasia. ” alieleza Mchambuzi wa siasa za Kimataifa na uhusiano wa Kimataifa Profesa Macharia Munene.

00:18

Mchambuzi wa siasa za Kimataifa na uhusiano wa Kimataifa Profesa Macharia Munene

Baada ya kuondolewa madarakani kwa Omar Hasan El Bashir, kulikuwa na jitihada zikiongozwa na Umoja wa Mataifa, ili kurejeshwa demokrasia mwaka 2023 lakini dalili zinaonesha kuwa itachukua muda mrefu.

Volker Perthes, mjumbe wa UN nchini Sudan alitangaza kujiuuzulu wiki hii
Volker Perthes, mjumbe wa UN nchini Sudan alitangaza kujiuuzulu wiki hii AFP - -

Mjumbe wa Umoja wa Mataifa, Perthes Volker, ambaye amekuwa akiongoza jitihada hizo alitangaza kujiuzulu siku ya Jumatano.

Taarifa ya mwandishi wetu wa masuala ya Sudan James Shimanyula.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.