Pata taarifa kuu

Sudan: Shambulio jipya la Anga  jijini Khartoum lawauwa takribani raia 20.

Nairobi – Nchini Sudan, katika jiji kuu Khartoum, watu zaidi ya 20 wakiwemo watoto wawili  wameuwawa baada ya shambulio la anga linalosemekana kutekelezwa na  la jeshi .

Moshi karibu na soko linalowaka moto huko Omdurman, kitongoji cha kaskazini mwa Khartoum, Mei 17, 2023.
Moshi karibu na soko linalowaka moto huko Omdurman, kitongoji cha kaskazini mwa Khartoum, Mei 17, 2023. © VIDEO OBTAINED BY REUTERS
Matangazo ya kibiashara

 

Kulingana na tarifa ni kuwa kuna baadhi ya miili iliyozikwa chini ya Vifusi katika eneo laKalakla al-Qubba kusini-magharibi mwa jiji hilo.

Taarifa za  awali,zimeonya  kuwa vifo zaidi havijarekodiwa, kwani miili  haiwezi kuhamishwa hospitalini kwa sababu ilichomwa vibaya .

Jeshi la serikali na lile la  wanajeshi wa Rapid Support Forces (RSF) wamekuwa wakipigania udhibiti wa mji wa Khartoum tangu Aprili  15 mwaka huu  huku watu milioni 2.2 wakitoroka makazi yao ndani ya Sudan na zaidi ya nusu milioni wakitafuta hifadhi katika nchi jirani, kulingana na Umoja wa Mataifa.

Kufikia sasa watu 5,000 wameuawa, kulingana na makadirio kutoka kwa mradi wa mahali pa vita na takwimu za tukio.

Vikosi vya Wanajeshi wa Sudan vinadhibiti anga na vimefanya mashambulio ya anga ya mara kwa mara huku wapiganaji wa RSF wakitawala mitaa ya mji mkuu.

Mzozo huo ulianza baada ya mkuu wa jeshi Jenerali Abdel Fattah al-Burhan na mkuu wa RSF Jenerali Mohamed Hamdan Dagalo kutofautiana kuhusu mustakabali wa nchi.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.